BERND HOLLERBACH AACHIA NGAZI HAMBURG SV.

Image result for Bernd Hollerbach
Baada ya  wiki  saba  madarakani  kocha  wa  Hamburg SV Bernd Hollerbach aachia  ngazi, safari ya kigogo hicho cha soka nchini  Ujerumani kuelekea daraja la pili nyeupee ..
Ni timu  ambayo  haijashuka daraja  tangu  Bundesliga  kuanzishwa  mwaka  1963. 
Imekwisha  kuwa  bingwa  wa  ligi ya  taifa  Bundesliga mara  6, kombe  la shirikisho DFB Pokal mara 3,  kombe  la washindi  barani  Ulaya, hivi  sasa  Europa League mara  1 na  Kombe  la  Ulaya , hivi  sasa  Champions League mara 1.
Timu  hii  ni  Hamburger SV  ambayo  kwa  jina  la  utani inaitwa  Dino, ama  Dinosaurus, wanyama  waliokuwa wakiishi  katika  dunia  miaka  milioni  kadhaa  iliyopita ambao  sasa  hawako  tena.
Misimu minne iliypopita  Hamburg SV imebadilisha  makocha  zaidi  ya kumi na  hakuna  hata  mmoja  aliyeonesha  kuiletea  uhai timu  hiyo licha ya kuiokoa  tu  dhidi  ya  kushuka  daraja. 
Lakini  msimu  huu  hali  inaonekana  kuwa  ngumu  zaidi kwani Kocha  Bernd Hollerbach aliyeteuliwa  kuiokoa  timu hiyo  naye  kibarua  kimeota  majani.
Hiyo  ndio historia  fupi ya  Hamburg SV ambayo  ni  ya mafanikio  makubwa  katika  soka  la  Ujerumani, timu ambayo  aliichezea pia  mchezaji  maafuru  wa  Ujerumani Kaiza Franz Beckenbauear  na  mchezaji  maarufu  wa Uingereza  Kevin Keegan. 
Lakini  hivi  sasa  imo katika hatari  ya  kushuka  daraja  la  pili na  kumekuwa  na mtafaruku  mkubwa  katika  timu  hiyo.
Hatua ya kumuondoa  Hollerbach  imekuja  baada  ya kichapo  cha  mabo 6-0 dhidi  ya  mabingwa  watarajiwa FC Bayern. 
Mchezaji  wa  Hamburg SV Sven Schipplock alisema  kocha  wa vijana  wa  umri  chini  ya  miaka  21  wa  klabu  hiyo Christian Titz  anatarajiwa  kutajwa  rasmi  kuwa  kocha  wa timu  ya  kwanza.


Share on Google Plus

About huhesofm blog

0 Comments:

Chapisha Maoni