TRUMP: SITISHENI VIZUIZI, TUONDOE USHURU.

Image result for TRUMP
Rais Trump wa Marekani amerudia madai yake kwamba Umoja wa Ulaya usitishe vizuwizi vyake vya biashara kwa biadhaa za Marekani ili kunusuru washirika wake hao na ushuru mpya wa chuma cha pua na bati.
Rais wa  Marekani  amesema  hayo  baada  ya  mazungumzo  magumu mjini  Brussels  kati ya wajumbe  wa  majadiliano  wa  Umoja  wa  Ulaya  na  mwakilishi  wa  masuala  ya biashara  wa Marekani Robert Lighthizer  katika  juhudi za  kumaliza  mzozo  mkubwa ambao  wengi  wanahofia  unaweza  kuingia  katika vita vikubwa  vya  kibiashara.
"Umoja  wa  Ulaya , mataifa  safi  kabisa ambayo  yanaitendea  Marekani  vibaya  kabisa katika  biashara, yanalalamika juu  ya  kodi katika  chuma cha  pua na  bati," Trump  alisema.Afisa  wa  ngazi  ya  juu  wa  biashara  wa  Umoja  wa  Ulaya  amesema  Marekani imeshindwa  kueleza  kwa  uwazi  juu  ya vipi Ulaya  na  Japan zinaweza  kuepuka kodi  hizo zinazotarajiwa  kuanza  wiki  ijayo.
"Iwapo wataondoa vizuwizi  vyao vibaya kabisa  na  kodi katika  biadhaa  za  Marekani zinazotozwa  hivi  sasa, tutafanya hivyo  hivyo  kuondoa  vyetu. Nakisi  kubwa. Iwapo hawatafanya  hivyo, tutaweka  kodi  kwa  magari. Haki!"
Tangazo la  rais Donald Trump  la  kuweka  ushuru wa  asilimia  25 kwa  chuma  cha  pua kitakachoingizwa  nchini  humo  na  asilimia  10 katika  madini  ya  bati limeuchoma Umoja wa  Ulaya, pamoja  na  washirika  wengine  wakubwa  ikiwa  ni  pamoja  na  Japan, ambayo waziri  wake  wa  uchumi Hiroshige Seko pia  alihudhuria  mazungumzo  hayo  mjini Brussels.
Share on Google Plus

About huhesofm blog

0 Comments:

Chapisha Maoni